GALATASARAY - PODOLSKI

Klabu ya Galatasaray imekamilisha usajili wa mshambuliaji wa Arsenal Lukas Podolski kwa mkataba wa miaka mitatu.
Mchezaji huyo mwenye uzoefu katika kikosi cha taifa, aliichezea mechi chache timu yake ya Taifa katika Kombe la Dunia ambapo Ujerumani waliibuka mabingwa. Mchezaji huyo alishindwa kuonesha cheche akiwa na klabu ya Arsenal na kujikuta akikosa namba kwenye kikosi cha kwanza na kumpelekea kusukumwa kwa mkopo katika klabu ya Inter ambapo alifanikiwa kufunga goli moja kwenye mechi 19.
Lakini mchezaji huyo mwenye miaka 30 anaimani yupo vizuri pia anaamini yupo mahali ambapo atarejesha heshima yake kwa kupambana na klabu za Ulaya ambazo zinashiriki Ligi ya Mabingwa na kutazamwa na mashabiki wengi.
"Mwaka uliopita Galatasaray walitoa ofa ya kunisajili," alisema Podolski. "Lakini mwaka huu kulikuwa na maslahi mazuri zaidi. Pia wazazi wangu walitaka nije hapa.
"Galatasaray walikuwa mabingwa mwaka jana.Tutapambana kuwa mabigwa katika miaka ijayo, sisi tunataka kupanda ngazi za juu zaidi.
"Nimekuwa nikiifuatilia Galatasaray kwa muda mrefu.Nafahamu kuna hali nzuri katika uwanja huo.
"Mashabiki wa Galatasaray wamenipa sapoti na wamefurahishwa na ujio wangu. Huu ni uamuzi mkubwa kwangu kwa kuamua jambo hili."
Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
PODOLSKI ATUA GALATASARAY RASMI...
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment