MANCHESTER UNITED - VAN PERSIE, SCHNEIDERLIN & RAMOS

Mshambuliaji wa Manchester United Robin Van Persie yupo kwenye hatua za mwisho za kujiunga na Fenerbahce baada ya kufikia makubaliano na klabu hiyo.
Chanzo: Guardian
Jumamosi, Julai 4, 2015 15:09

Manchester United wanajiandaa kutoa ofa ya pili kwa ajili ya Morgan Schneiderlin baada ya klabu ya Southampton kukataa ofa ya awali £20m.
Chanzo: Guardian
Jumamosi, Julai 4, 2015 10:22

Haijalishi ni kiasi gani cha pesa klabu ya Real Madrid watatoa kwa Sergio Ramos, Mhispania huyo ana nia ya kuondoka. Mchezaji huyo mwenye miaka 29 anahisi kuondoka Bernabeu na mwenyewe anahitaji kupata uzoefu katika ligi kuu na anahitaji kujiunga na Manchester United.
Chanzo: Marca
Jumamosi, Julai 4, 2015 00:14
CHELSEA - JUAN CUADRADO & GERSON

Klabu ya Chelsea imeamua kumbakiza Juan Cuadrado msimu huu japo mchezaji huyo hakuwa na mwanzo mzuri katika kipindi alichokuwa Stamford Bridge.
Chanzo: EL PaĆs
Jumamosi, Julai 4, 2015 13:57

Chelsea wameanza mazungumzo na klabu ya Fluminense juu ya uwezekano wa kumsajili kiungo wa klabu hiyo Gerson. klabu ya Juventus tayari imeandaa ofa ya euro milioni 17(£12.1m) kwa ajili ya mchezaji huyo mwenye miaka 18, wakati klabu za Manchester United na Barcelona zimeonesha nia ya kumuhitaji mchezaji huyo pia.
Chanzo: Tuttosport
Jumamosi, Julai 4, 2015 07:47
PSG - KEVIN TRAPP & PATRICK ROBERTS

Kevin Trapp amefikia makubaliano binafsi na klabu ya PSG kwa ajili ya uhamisho wake msimu huu, hata hivyo mabigwa hao wa Ufaransa bado wanakibarua kigumu kwani wanahitaji kuishawishi klabu ya Eintracht Frankfurt kukubali mpango huo wa kumsajili mlinda mlango huyo.
Chanzo: Bild
Jumamosi, Julai 4, 2015 08:39

Paris Saint-Germain wameonesha nia ya kumsajili mshambuliaji wa Fulham Patrick Roberts. Manchester City pia imeweka nia hiyo kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 18.
Chanzo: Daily Mail
Jumamosi, Julai 4, 2015 00:00
ARSENAL & LIVERPOOL - PEDRO

Klabu za Arsenal na Liverpool zimezungumza na wakala wa Pedro kuhusu uwezekano wa kumsajili mshambuliaji huyo wa Barcelona. Mchezaji huyo mwenye miaka 27anatarajia kwenda Uingereza, pia Paris Saint-Germain wameonesha nia ya kumsajili mchezaji huyo.
Chanzo: Sport
Jumamosi, Julai 4, 2015 07:58
ATLETICO MADRID - NICO GAITAN & SANTI CAZORLA

Atletico Madrid wanakaribia hatua za mwisho za mazungumzo na klabu ya Benfica kuhusu uwezekano wa kumsajili Nico Gaitan lakini klabu hiyo ya Ureno inahitaji dau la euro milioni 35(£24.9m).
chanzo: Record
Jumamosi, Julai 4, 2015 10:24

Klabu ya Atletico Madrid itarudi kwa kasi kuangalia uwezekano wa kumsajili Santi Cazorla mara baada ya kuondoka kwa Arda Turan. Diego Simeone alimuwania Mhispania huyo zaidi ya miaka miwili lakini klabu ya Arsenal inahitaji ofa kubwa kwa ajili ya mchezaji huyo.
Chanzo: Daily Mail
Jumamosi, Julai 4, 2015 00:23
Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
VAN PERSIE KUONDOKA UNITED,CAZORLA ASAKWA NA ATLETICO,CHELSEA WAMNYATIA GERSON...
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment