DROGBA APEWA OFA MLS:

Klabu ya MLS imempatia ofa ya mkataba nyota mkongwe wa chelsea Didier Drogba, huku Chicago Fire wakiongoza mbio za kuiwania saini ya mshambuliaji huyo wa zamani wa Chelsea. Hata hivyo kuna upinzani kutoka klabu ya Qatari.
Chanzo: ESPN
Ijumaa,7/17/2015 22:21
ARSENAL WAJIANDAA KUTOA DAU KWA AUBAMEYANG:

Arsenal wanajiandaa kutoa ofa kwa mchezaji wa klabu ya Borussia Dortmund Pierre-Emerick Aubameyang. Klabu hiyo ya Bundesliga wanataka pauni milioni 31 kwa ajili ya mshambuliaji huyo.
Chanzo: Reviersport
Ijumaa,7/17/2015 14:02
EVERTON WAHITAJI ADA YA REKODI YA UINGEREZA KWA STONES:

Everton wameitaka klabu ya Chelsea kulipa ada ya rekodi ya Uingereza kama wanahitaji saini wa beki wa klabu hiyo John Stones. Kwa sasa klabu ya Manchester City inashikilia rekodi hiyo ya pauni milioni 31.9 iliyomtolea Eliaquim Mangala.
Chanzo: Daily Mirror
Ijumaa,7/17/2015 22:45
MAN UTD WANAJIPANGA KUMNYAKUA PEDRO:

Manchester United wanajipanga kutoa ofa ya euro milioni 31.5 sawa na pauni milioni 22 kwa ajili ya kumnyaka mchezaji wa Barcelona Pedro na wanamatumaini ya kuipiku klabu ya Chelsea katika harakati za kuiwania saini ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27.
Chanzo: Daily Mirror
Ijumaa,7/17/2015 22:35
SOUTHAMPTON WANAKARIBIA KUMPATA VLAAR BAADA YA LAZIO KUJITOA:

Southampton wanakaribia kumnyaka beki wa Aston Villa Ron Vlaar baada ya klabu ya Lazio kujitoa kwenye mbio za kumuwania mchezaji huyo.
Chanzo: Daily Express
Ijumaa,7/17/2015 20:18
BRADY ANAKARIBIA KUJIUNGA NA NORWICH:

Robbie Brady amekataa dili jipya na Hull City huku akiwa anakaribia kujiunga na Norwich kwa ada ya pauni milioni 7.
Chanzo: Daily Mirror
Ijumaa,7/17/2015 20:14
ROMA INAMUWANIA MORENO:

Roma wanajipanga kumuwania mchezaji wa Liverpool Alberto Moreno. Walter Sabatini yupo Uingereza kukamilisha usajili wa Edin Dzeko na pia anataraji kukutana na maofisa wa Liverpool kuzungumzia ofa ya euro milioni 11.5 (Pauni milioni 8) kwa ajili ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23.
Chanzo: Daily Express
Ijumaa,7/17/2015 19:38
MAN UTD WAKATAA KUMUUZA DE GEA BILA RAMOS:

Manchester United wamejiengua wenyewe kutokana na kumpoteza mlinda mlango wao David De Gea ama majira haya ya joto au yajayo, hata hivyo watamuuza kwa kilabu cha Real Madrid kama Sergio Ramos atakuwa sehemu ya makubaliano.
Chanzo: Sky Sports
Ijumaa,7/17/2015 18:09
PORTO WADONDOSHA OFA KWA MITROVIC:

Porto wametoa ofa ya pauni milioni 12.5 katika klabu ya Anderlecht ili kumnyakuwa mshambuliaji wao Aleksander Mitrovic baada ya dau la Newcastle kwa ajili ya mchezaji huyo kukubaliwa. Chelsea pia wameonesha nia kwa mchezaji huyo.
Chanzo: Daily Mirror
Ijumaa,7/17/2015 17:50
Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
TETESI ZA USAJILI BARANI ULAYA...
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment