ARSENAL-EDIN DZEKO:

Arsenal wanatazamia kumnyakuwa mshambuliaji wa Manchester City Edin Dzeko huku kukiwa na wasiwasi wa bosi wa Arsenal kumtegemea sana Olivier Giroud. Mshambuliaji huyo pia ameivutia klabu ya Roma lakini ana nia ya kuendelea kubaki katika Ligi Kuu ya Uingereza.
Chanzo: Daily Star
Jumapili,7/19/2015 08:21
MAZUNGUMZO YA DI MARIA NA PSG YAMESIMAMA:

Usajili wa Angel Di Maria kutoka klabu ya Manchester United kwenda PSG umesimama huku kukiwa na ubishani wa ada ya uhamisho wa mchezaji huyo kati ya vilabu hivyo viwili. Margentina huyo tayari amekwisha kubaliana masharti na mabingwa hao wa Ufaransa, ambao pia wametupia jicho lao kwa Kevin De Bruyne.
Chanzo: L'Equipe
Jumapili,7/19/2015 08:18
MAN UTD BADO INAMNYEMELEA BALE:

Manchester United bado hawajakatisha matamanio yao ya kumnyakuwa mchezaji wa Real Madrid Gareth Bale, huku Louis van Gaal akipanga kufanya jaribio lingine la kumleta mchezaji huyo wa taifa wa Wales.
Chanzo: Sunday Mirror
Jumamosi,7/19/2015 22:43
STAMBOULI ANAKARIBIA KUJIUNGA NA PSG:

Kiungo wa Tottenham Benjamini Stambouli yupo USA kusaini dili la mkataba wa miaka mitano na klabu ya PSG. Usajili huo utatangazwa rasmi siku ya Jumapili au Jumatatu.
Chanzo: Le Parisien
Jumapili,7/19/2015 11:31
SALAH AKUBALI KUTUA ROMA KWA MKOPO:

Mohamed Salah anajipanga kujiunga na klabu ya Roma kwa mkopo baada ya kukubali kuelekea Serie A. Roma wameipatia klabu ya Fiorentina Matta Destro kama fidia wakati Chelsea wakimuhitaji Alessio Romagnoli kama sehemu ya dili hilo.
Chanzo: Daily Mail
Jumapili,7/19/2015 10:42
ASTON VILLA INAMTAKA CALLUM KAMA MBADALA WA BENTEKE:

Aston Villa wanampango wakumnyakuwa mshambuliaji wa Bournemouth Callum Wilson kama mbadala wa Christian Benteke. Mshambuliaji huyo ataigharimu timu hiyo inayonolewa na Tim Sherwood pauni milioni 7.
Chanzo: Daily Express
Jumapili,7/19/2015 09:40
Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
DONDOO ZA USAJILI MAJUU...
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment