MANCHESTER UNITED - THOMAS MULLER , MATTEO DARMIAN & RAMOS

Manchester United wanajiandaa kutoa ofa ya euro milioni 82(£58m) kwa ajili ya Thomas Muller. Mh Woodward anatarajia kuzungumza na Karl-Heinz Rummenigge juu ya uwezekano wa kukamilisha dili hilo.
Chanzo: Sport1
Jumanne, Julai 7, 2015 00:09

Mazungumzo baina ya Manchester United na Torino yanaendelea vizuri baada ya Mashetani Wekundu hao kukaribia kumnyakua Matteo Darmian. Dili hilo la euro milioni 14 litafanyika haraka, huku Louis van Gaal akiwa tayari kumsajili beki huyo wa kulia.
Chanzo: Gianluca di Marzio
Jumanne, Julai 7, 2015 00:47

Manchester United wameiambia klabu ya Real Madrid kwamba David De Gea hatoweza kwenda Santiago Bernabeu ikiwa Sergio Ramos bado yupo klabuni hapo. Mashetani wekundu hao wamesema watamuachia golikipa huyo endapo watampata beki huyo wa kati.
Chanzo: Manchester Evening News
Jumanne, Julai 7, 2015 00:07
PSG - KEVIN DE BRUYNE

Paris Saint-Germain wameingia kwenye mbio za kumuwania nyota wa Wolfsburg Kevin De Bruyne. PSG walifanya mazungumzo na mchezaji huyo wa ubelgiji mwishoni mwa wiki, lakini klabu ya Manchester City bado wanamatumaini ya kumnyakua mchezaji huyo kwa ada ya euro milioni 70.
Chanzo: Daily Mail
Jumanne, Julai 7, 2015 00:27
BAYERN MUNICH - DI MARIA

Klabu ya Bayern Munich wanajiandaa kutoa ofa kambambe kwa nyota wa Manchester United Angel Di Maria. Bavariani hao watamtoa mchezaji anayesakwa kwa mda mrefu Thomas Muller pamoja na winga Arjen Robben kwa ajili ya kumpata mchezaji huyo aliyevunja rekodi ya usajili nchini Uingereza.
Chanzo: Daily Mail
Jumanne, Julai 7, 2015 00:47
ARSENAL - EDUARDO VARGAS

Klabu ya Arsenal imerejea kwenye mchakato wa kumnyakua Eduardo Vargas kwa lengo la kuunda uhusiano na mchezaji mwenzake wa Chile Alexis Sanchez.
Chanzo: Corriere dello Sport
Jumanne, Julai 7, 2015 10:32
REAL MADRID - ZLATAN IBRAHIMOVIC

Real Madrid wanafuatilia kwa karibu uhusiano kati ya Zlatan Ibrahimovic na klabu yake ya Paris Saint-Germain. Madrid wapo tayari kutoa mkataba wa miaka mitatu wenye thamani ya euro milioni 12(£8.4m) kwa msimu lakini hawawezi kutoa ofa itakayozidi euro milioni 6(£4.2m) kwa mchezaji huyo menye miaka 33.
Chanzo: Sport
Tuesday, July 7, 2015 10:38
TOTTENHAM - TOBY ALDERWEIRELD

Toby Alderweireld amefaulu vipimo vya matibabu katika klabu ya Tottenham ambapo mchezaji huyo anatarajia kujiunga na timu hiyo akitokea Atletico Madrid kwa ada ya £11.5m.
Chanzo: talkSPORT
Jumanne, Julai 7, 2015 14:01
PORTO - IKER CASILLAS

Porto wametoa mkataba wenye ofa ya miaka miwili kwa Iker Casillas, kukiwa na kigezo cha mwaka mmoja mbele, na thamani ya euro milioni 5 kwa msimu. Real Madrid wanampango wa kumuachia mchezaji huyo aondoke bure lakini watakuwa hawajafikia ada ya makazi kwa ajili ya miaka miwili iliyobaki.
Chanzo: Marca
Jumanne, Julai 7, 2015 12:52
LIVERPOOL & TOTTENHAM - KEMEN

Liverpool na Tottenham wapo kwenye kinyang'anyiro cha kumsajili kiungo wa Newcastle United mwenye miaka 18 Olivier Kemen
Chanzo: L'Equipe
Jumanne, Julai 7, 2015 11:33
ROMA - EDIN DZEKO

Edin Džeko amekubaliana na klabu ya Roma ili mchezaji huyo ahamie klabuni hapo ambapo atapewa mkataba wa miaka minne na kupokea euro milioni 4.5 kwa msimu lakini klabu hiyo ya Serie A bado hawajakutana na klabu ya Manchester City kujadili uwezekano wa kumsajili mchezaji huyo kwa ada ya euro milioni 25.
Chanzo: Calciomercato.com
Jumanne, Julai 7, 2015 11:01
INTER - IVAN PERISIC

Klabu ya Inter ipo tayari kumtoa Xherdan Shaqiri kwa ajili ya kupata saini ya Ivan Perisic. Tottenham , Stoke City na Atletico Madrid wote wamekuwa wakimnyatia mchezaji huyo wa kimataifa wa Uswisi.
Chanzo: Corriere dello Sport
Jumanne, Julai 7, 2015 10:34
VALENCIA - VICTOR VALDES

Golikipa wa Manchester United Victor Valdes ametanabaisha kukataa ofa ya Valencia. Golikipa hiyo mwenye miaka 33 anaimani atakuwa chaguo la kwanza mbele ya Louis van Gaal kama David De Gea ataondoka klabuni hapo.
Chanzo: AS
Jumanne, Julai 7, 2015 11:49
NAPOLI - JOSE CALLEJON

Wakala wa Jose Callejon amepanga kukutana na raisi wa Napoli Aurelio De Laurentiis ili waweze kujadili mustakabali wa mchezaji huyo mwenye miaka 28. Klabu ya Atletico Madrid imeonesha nia ya kumsajili mshambuliaji huyo ambaye thamani yake ni kati ya euro milioni 20(£14.2m) na euro milioni 25( £ 17.7m ).
Chanzo: Mediaset
Jumanne, Julai 7, 2015 00:00
Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
UNITED YAREJEA KWA MULLER,MADRID YAMSAKA IBRAHIMOVIC,ARSENA YARUDI TENA KWA VARGAS...
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment