Goal inakuletea dondoo mbali za usajili za nyumbani na kwingineko duniani
Sterling hajaonekana mazoezini Liverpool kwa siku mbili mfululizo
Raheem Sterling ambaye amadhamiria kuihama timu yake msimu huu hajaonekna katika mazoezi ya timu hio kwa kisingizio kwamba anaumwa, Je uhamisho wake umekaribia?Ramadhani Singano yuko huru kujiunga na timu yoyote
Shirikisho la soka Tanzania limethibitisha kuwa mchezaji Ramadhani Singano ‘Messi’ kuwa yupo huru na anaweza kusajiliwa na timu yeyote itakayo muhitaji baada ya klabu yake aliyokuwa akiichezea siku za nyuma Simba kushindwa kutekeleza baadhi ya vipengele vilivyopo kwenye mkatabaManchester United kumsajili Darmian, akiri kocha wa Torino
Manchester United wanakaribia kukamilisha usajili wa beki wa kimataifa wa Italy Matteo Darmian, uhamisho huo ulithibitishwa na kocha mkuu wa Torino Giampiero Ventura aliyekiri kuwa uhamisho huo uko mbioni kukamilikaTanzania yajitoa All Africa Games
Katibu mkuu wa Kamati ya Olimpiki nchini Tanzania (TOC), Filbert Bayi amesema uongozi wa chama hicho umeitaarifu kamati yake juu ya kutoshiriki michuano hiyo itakayoanza September 4-19.Ukosefu wa fedha umekuwa ni kikwakzo kwa vyama vingi vya michezo nchini Tanzania kushiriki katika michezo mbalimbali ya kimataifa ikiwemo ya kufuzu michuano mbalimbali ikiwemo hiyo ya Afrika na mengineyo kama vile ya Olimpiki na Jumuiya ya Madola.
Serikali inategemewa kugharamia ushiriki wa wanamichezo kuelekea katika michezo hiyo lakini mpaka sasa haijajulikana ni wanamichezo wangapi watashirki.
Mbali ya baiskeli, Tanzania inategemewa kushiriki katika michezo ya taekwondo, kuogelea, riadha, ngumi na michezo ya watu wenye ulemavu.
Wachezaji wa kimataifa wawasili Azam
Azam ilimaliza nafasi ya pili katka msimu wa ligi uliokwisha na kupata tiketi ya kuiwakilisha Tanzania katika michuano ya Shirikisho. Mmoja wachezaji hao ni mlinda lango Mkameruni anayekipiga nchini Congo (DRC ), Nelson Lukong, anayetegemewa kusaili usiku huu.Mbali na Nelson Lukong leo Alhamisi saa mbili asubuhi kiungo toka nchini England Ryan Burge atawasili na Qatar Air.
Jean Mugiraneze Babtiste toka nchini Rwanda anayekipiga na APR atawasili na Rwanda Air jioni ya leo Alhamisi.
Baada ya mazoezi ya wiki tatu Azam FC inasafiri leo asubuhi kuelekea mjini Tanga, Kaskazini mwa Tanzania kucheza mechi mbili za kirafiki. Itacheza na African sports wana kimanumanu siku ya Jumamosi na Jumapili itakwaana na Coastal Union Mechi zote mbili zitachezwa kwenye uwanja wa CCM Mkwakwani majira ya jioni.
Timu itarejea Dar es Salaam siku ya Jumatatu.
Kocha Wa Taifa Stars awashukuru watanzania
Mkwasa amesema kujitolea kwa wachezaji wa Taifa Stars (uzalendo) katika mchezo huo kulipelekea kuwapa wakati mgumu wenyeji, huku watanzania waliojitokeza kuja kushuhudia mchezo huo wakiwashangilia muda wote wa mchezo. Uganda (The Canes) ilitoka sare ya 1-1 katika mchezo huo na kusonga mbele kwa jumla ya magoli 4-1.“Kiukweli japo timu haikuweza kupata matokezo mazuri sana, lakini tunamshukuru Mungu ndani ya wiki moja ya maandalizi, tumeweza kuwapa maelekezo vijana na kuyafanyia kazi, japo wengine walikua wakicheza kwa mara ya kwanza timu ya Taifa walicheza vizuri, kijumla wote kwa pamoja walifanya vizuri sana katika mchezo dhidi ya Uganda” alisema Mkwasa.









0 comments:
Post a Comment