
Klabu ya Barcelona imekamilisha usajili wa mchezaji wa Atletico Madrid Arda Turan baada ya mchezaji huyo kusaini mkataba wa miaka mitano na klabu hiyo siku ya Ijumaa.
Wiki iliyopita klabu ya Barcelona ilikubaliana na Atletico Madrid ada ya euro milioni 41 kwa ajili ya mchezaji huyo wa kimataifa wa Uturuki, japokuwa Barcelona wana haki ya kuukataa uhamisho huo kwa gharama ya euro milioni 4.1 kama mrithi wa Josep Maria Bartomeu ataingia madarakani kwa kuwa anadhani Arda hana nafasi katika kikosi hicho.
Hata hivyo, Arda Turan amesisitiza kuwa haogopi kurudishwa kwenye klabu yake ya Vicente Calderon (Atletico Madrid).
"Sina wasi wasi, mimi ni mcheza mpira," mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28 aliwaambia waandishi wa habari siku ya Ijumaa. "Nipo hapa kuisaidia Barcelona ipate mafanikio zaidi. Vitu vingine sio vyangu kuhofia."
Arda pia aliutupilia mbali uvumi kuwa yeye ndiye mrithi wa Xavi aliyetimka klabuni mapema baada ya msimu 2014-2015 kuisha kujiunga na klabu ya Al Sadd.
"Kwanza kabisa, hakuna anayeweza kuwa mrithi wa Xavi kwa kuwa ni mchezaji bora," aliongezea winga huyo. "Alikuwa ni nyota na utambulisho wa Barcelona na Hispania."
"Mimi ni mchezaji tofauti. Mimi sio Xavi. Lakini nitajaribu kusaidia kwa uwezo wangu binafsi na staili yangu."
Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
ARDA TURAN ATUA BARCELONA RASMI...
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment