VAN GAAL AITAKA MAN UTD KUMUUZA DE GEA:

Meneja wa kilabu cha Manchester United Louis van Gaal kwa sasa anaitaka klabu hiyo kumuuza David De Gea kwa Real Madrid kwa kuwa mawazo ya golikipa huyo yameathiriwa na makubaliano kati ya vilabu hivyo.
Chanzo: AS
Jumamosi, 8/1/2015 09:46
MAN CITY WANAJIPANGA KUMNYAKA PEP KWA £100M:

Manchester City wanaamini kuwa watamnyaka kocha wa Bayern Pep Guardiola kwa dau la kushangaza la pauni milioni 100. Bosi huyo wa Bayern Munich, ambaye anaonekana kuwa tayari kuhama Ujerumani, anajipanga kuchukuwa nafasi ya Manuel Pellegrini msimu ujao kwa mkataba wa pauni 20 milioni kwa msimu.
Chanzo: The Sun
Jumamosi, 8/1/2015 00:02
DI MARIA AMEKUBALIANA VIGEZO NA PSG:

Angel Di Maria amepiga hatua karibu na kujiunga na PSG baada ya kukubaliana vigezo binafsi, huku Margentina huyo akitegemewa kukamilisha vipimo vya afya mapema wiki ijayo. Winga huyo atasaini mkataba wa miaka minne wenye thamani ya euro milioni 10.5 kwa msimu na bei ya uhamisho waliyokubaliana na Manchester United ni euro milioni 63.
Chanzo: TRMC
Ijumaa, 7/31/2015 21:54
INLER AITOLEA NJE LEICESTER:

Kiungo wa Napoli Gokhan Inler amekataa kuhamia Leicester City. Vilabu hivyo vimekubaliana ada ya euro milioni 4 (£2.8m).
Chanzo: Sky Sport Italia
Jumamosi, 8/1/2015 09:45
BERBATOV AFANYA MAZUNGUMZO NA ASTON VILLA:

Dimitar Berbatov atasafiri kuelekea Birmingham siku ya Jumatatu kufanya mazungumzo ya ana kwa ana na bosi wa Aston Villa Tim Sherwood juu ya uhamisho uliopendekezwa. Villa wanataka kuongeza nguvu katika nyanja ya ushambuliaji na huenda dili hilo likakamilika ndani ya wiki.
Chanzo: Daily Express
Ijumaa, 7/31/2015 21:43
AKPOM KUJIUNGA NA HULL CITY KWA MKOPO:

Licha ya kusisitiza kuwa hatotolewa kwa mkopo, Arsene Wenger amekubali kumtoa kwa mkopo Chuba Akpom kwa kilabu cha Hull City kwa kampeni ya 2015-2016. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 19 licha ya kuonesha makali katika michezo ya maandalizi ya msimu anajipanga kushiriki Championship.
Chanzo: BBC
Ijumaa, 7/31/2015 20:19
Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
TETESI ZA USAJILI ULAYA: LVG AITAKA MAN UTD IMUUZE DE GEA HARAKA, GUARDIOLA KUTUA MAN CITY KWA £100M...
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment