
Kocha Arsene Wenger amesema staa wa Chelsea, Eden Hazard hajafikia kiwango cha kuanza kumwingiza kwenye kundi la mafundi kama Lionel Messi na Cristiano Ronaldo.
Wenger alisema hata nyota wake kwenye kikosi cha Arsenal, Alexis Sanchez anaweza kumfunika Hazard katika msimu huu.
Akizungumza na ESPN, kocha huyo Mfaransa alisema: “Labda ukiniambia ni maoni tu ya mtu hapo sawa. Kama kwa kulinganisha namba tu, naweza kusema Messi na Ronaldo wanafunga hadi mabao 50 na kuwa peke yao. Hakuna mpinzani. Sitaki kuzungumzia hilo. Kila mtu nafikiri anadhani mchezaji wake ni bora kitu ambacho kinaeleweka tu. Nikimtazama Sanchez kwa kitu ambacho amekifanya katika msimu wake wa kwanza Ligi Kuu England ni cha kipekee.
“Nina imani hatarudia tu, bali ataongeza zaidi. Hazard anaweza kubadili mechi na utaweza tu kumweka daraja hilo kama atafanya hivyo mara kwa mara.”

Arsenal na Chelsea watamenyana siku ya kesho katika mchezo wa ngao ya hisani huku wadau wa soka duniani wakiamini huenda Wenger akapata ushindi wake wa kwanza mbele ya vijana wa Jose baada ya kumnyakuwa mlinda mlango mahiri Petr Cech kutoka katika kilabu hicho pinzani msimu huu.
Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
WENGER: SANCHEZ NI BORA KULIKO HUYO HAZARD
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment