
Wakala wa mshambuliaji wa Porto Jackson Martinez ana matumaini kwamba mchezaji huyo wa kimataifa wa Colombia atajiunga na klabu ya AC Milan. Klabu hizo mbili zipo mbioni kufikia makubaliano juu ya mchezaji huyo, alifafanua wakala huyo.
Klabu ya AC Milan inatarajia kuanza kujijenga vema baada ya kumaliza nafasi ya 10 msimu uliomalizika wa Serie A, kutokana na bajeti kubwa iliyopatikana kutoka kwa uwekezaji wa mfanyabiashara wa Thailand Bee Taechaubol katika klabu hiyo.
Uhusiano wa Martinez kujiunga na klabu hiyo umeenea haraka kukiwa na uvumi kwamba klabu hiyo ina nia ya kumrejesha mshambuliaji wake wa zamani Zlatan Ibrahimovic, na sasa wakala wa mchezaji huyo wa kimataifa wa Colombia ameisifia Milan kuwa ni klabu kubwa.
"Nina matumaini juu ya uhamisho wa Jackson kwenda Milan, lakini bado hatuna uhakika," Luiz Henrique Pompeo aliiambia EuroStadio. "Kuna uwezekano mkubwa uhamisho huo ukatimia, lakini bado hatupo kwenye hatua ya kuweka mambo wazi kwa sasa."
"Ninachoweza kusema kwa hakika ni kwamba Martinez ni mchezaji anayestahili klabu ya juu kama Milan yenye historia."
"Je, watalipia €35,000,000? ni swala la kuwauliza Milan, sio swala la upande wetu. Kuhusu mshahara, siwezi kujadili takwimu kwa sasa. Lakini bado hakuna makubaliano na mchezaji huyo."
Klabu ya Porto imepanga kupata faida kubwa kutokana na mauzo ya mchezaji huyo wa kimataifa wa Colombia ambaye alisaini klabuni hapo mwaka 2012 kwa dau la €9m kama mbadala wa washambuliaji Radamel Falcao na Hulk waliotimka klabuni hapo.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28 amethibitisha ubora wake katika klabu hiyo ya Estadio do Dragao kwa kupachika magoli 92 katika michezo 133 aliyowachezea miamba hao wa Ureno.
Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
JACKSON MARTINEZ ATIMKIA AC MILAN
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment