
Manchester United imethibitisha usajili wa mchezaji Memphis Depay kutoka PSV kwa ada ya Euro milioni 30.8 uliokamilika mwanzoni mwa mwezi wa tano licha ya kuwepo kwa upinzani kutoka kwa klabu ya Liverpool iliyoonesha nia ya kumtaka mchezaji huyo.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 21 alikubali kuhamia Old Trafford mapema mwezi wa tano kabla ya dili kuthibitishwa rasmi siku ya Ijumaa.
Tovuti ya Goal imetabanaisha kwamba msimu uliopita kocha wa klabu ya Manchester United Louis van Gaal alizungumza na Depay akimshauri kubaki PSV kwa mwaka mmoja zaidi kabla ya kuhamia Old Trafford, na baada ya kushinda kampeni za Eredivisie, hatimaye mshambuliaji huyo amesaini rasmi mkataba wa miaka minne na klabu ya Man Utd.

Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Uholanzi alisema,"Kwangu mimi hii ni kama ndoto iliyokuwa kweli; kucheza katika klabu kubwa duniani na kupata nafasi ya kufanya kazi na mtu ambaye binafsi naamini ni kocha bora duniani Louis van Gaal.
"Nina imani kubwa sana na uwezo wangu na nitafanya kazi kwa bidii kuweza kukamilisha ndoto zangu.
"Nimekuwa na PSV Eindhoven tangu nikiwa na umri wa miaka 12 na ninapenda kuwashukuru kwa kila kitu. Ulikuwa ni wakati wa furaha sana pale tuliposhinda ligi na nilifurahi sana kuwa sehemu ya furaha hiyo. Huu sasa ni ukurasa mpya katika maisha yangu na niliokuwa nikiutegemea.
Louis van Gaal aliyemchukua Depay kwenye Mashindano ya Kombe la Dunia mwaka 2014 kama sehemu ya kikosi cha Uholanzi amesema: " Ninamfahamu Memphis vizuri tangu kipindi tunafanya kazi pamoja katika timu ya taifa ya Uholanzi. Ni kijana ambaye anaweza kucheza nafasi tofauti uwanjani.

"Itamchukuwa muda Memphis kuendana na ligi ya Uingereza lakini sina shaka ana vigezo vya kuwa mcheza mpira mashuhuri kwa klabu yake na yupo katika klabu inayofaa kuendeleza kazi nzuri ambayo amekwishaifanya."
Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
MEMPHIS DEPAY ATUA RASMI OLD TRAFFORD....
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment