
Raisi wa klabu ya Real Madrid Florentino Perez anasema klabu hiyo itathibitisha kuwa wanaweza kufanya "Haiwezekani" kuwezekana msimu ujao.
Klabu hiyo ya Madrid ilishinda taji la Ligi ya Mabingwa Barani Ulaya pamoja na Copa del Rey mwaka 2014 lakini hawakuweza kulilinda kombe hilo msimu uliopita pamoja na kukosa kikombe cha ligi na hivyo kunyakuliwa na wapinzani wao klabu ya Barcelona.
Ukosefu wa mataji katika klabu hiyo umepelekea uamuzi wa klabu hiyo kumtupia virago kocha wao wa zamani Carlo Ancelotti na baadae kumteua Rafa Benitez kama mrithi wake na kumfanya Perez kuwa na matumaini kwamba klabu hiyo itarejea katika makali yake ya awali.
"Tutarudi katika hali yetu ya mapambano muda si mwingi," alisema katika hotuba kutoka VIP box Santiago Benabeu siku ya Jumanne.
"Hiyo ndio njia pekee tumeweza kuonesha ya kuwa ndoto zinaweza kufikiwa, zozote zile, zinazowezekana na zinazoonekana kutowezekana."
"Katika klabu hii unajifunza kutokukata tamaa katika mchezo kama sababu ya kupotea, kupambana hadi sekunde ya mwisho na kurudi tena na nguvu pale tunapopata matokeo tusiyoyahitaji."
Benitez amekuwa kocha wa nne tangu Perez alipochaguliwa kama raisi wa klabu hiyo mnamo mwaka 2009, kipindi ambacho wameonekana wakipata taji moja tu la Ligi.
Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
PEREZ: KISICHOWEZEKANA KITAWEZEKANA MSIMU UJAO...
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment