
Pamoja na mchezo wa soka kukumbwa na kashfa kubwa, soka la Barani Ulaya limeelekeza macho yake katika mafanikio chanya zaidi.
Ufaransa inaadhimisha mwaka mmoja kuelekea fainali za UEFA Euro 2016 zitakazofanyika katika mji wa mkuu wa Paris.
Rais wa Ufaransa François Hollande amempokea Raisi wa mpira wa miguu wa Barani Ulaya Mfaransa mwenzake Michel Platini katika Elysée Palace kuadhimisha tukio hilo.
Michel Platini amekuwa mtu wa kwanza kupokea tiketi kwa ajili ya mashindano hayo ya #EURO2016 kutoka kwa rais wa Ufaransa François Hollande.
Kwa sasa tiketi hizo kwa ajili ya mashindano hayo ya #EURO2016 zimeanza kuuzwa.
Lakini pamoja na hali nzuri ya mazingira ya mji mkuu wa Paris, kuna wasiwasi kuhusu gharama za mashindano, kifedha na katika suala zima la sifa pia.
Uvumi mkubwa unaoenea kwamba Platini anaweza kuwania nafasi ya uraisi wa FIFA kutokana na raisi wa zamani Sepp Blatter kuachia ngazi hiyo siku za karibuni kutokana na kashfa za rushwa.
Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
TIKETI ZA UEFA EURO 2016 KUANZA KUUZWA...
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment