CHELSEA-ALEX SONG

Chelsea imeingia kwenye mbio za kumsajili kiungo wa klabu ya Barcelona Alex Song. West Ham wanajaribu kupata saini ya mchezaji huyo wa kimataifa wa Cameroon kwa uhamisho huru, lakini Chelsea huenda ikatoa dau la £5m amabazo zinahitajika na klabu ya Barca kama Jose Mourinho anahitaji kuimalisha safu ya kiungo.
LIVERPOOL-FERNANDO LLORENTE & CARLOS BACCA

Baada ya kushindwa kufikia makubaliano na klabu ya Aston Villa ya £ 32,500,000 kama ada ya mchezaji Christian Benteke,Liverpool wanataka kumsajili mshambuliaji wa Juventus Fernando Llorente na mchazaji wa Sevilla Carlos Bacca.
MANCHESTER UNITED-DAYOT UPAMECANO

Manchester United wameipiku klabu ya Arsenal kwa kumsaini beki wa Valenciennes Dayot Upamecano mwenye umri wa miaka 16. Kijana huyo ataungana na wenzake katika kikosi cha United cha vijana.
ARSENAL-CARL JENKINSON

Arsenal wanatarajia kumpa mkataba mpya beki wa kulia Carl Jenkinson klaba ya kumpeleka mchezaji huyo kwa mkopo kwa awamu nyingine, baada ya beki huyo wa kulia kuichezea West Ham kwa msimu wa 2014-15.
Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
SONG KUELEKEA CHELSEA,CARL JENKINSON AONGEZWA MKATABA ARSENAL,MAN UNITED YAIPIKU ARSENAL KWA DAYOT ,LIVERPOOL WAMSAKA FERNANDO LLORENTE & CARLOS BACCA........
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment