
Kwa sasa mchezaji wa kimataifa wa Argentina na klabu ya Barcelona Lionel Messi atakuwa amezoea kukutana na maombi ya "selfies" kutoka kwa wachezaji na hata mashabiki.
Argentina iliwapiga Jamaica 1-0 Jumamosi ili kujipatia nafasi ya juu ya kundi B katika mashindano ya Copa America, lakini inaonesha wapinzani hao timu ya taifa ya Jamaica waliyafurahia matokeo hayo zaidi kuliko washindi wa mchezo huo Argentina.
Messi, ambaye alikuwa tayari ameombwa jezi yake wakati wa mapumziko, alionekana kutopendezwa na matokeo hayo wakati akitoka nje ya uwanja baada ya mchezo kumalizika, lakini bado alichukua muda wake kukaa na Deshorn Brown baada ya kumpatia jezi yake ya pili ya mchezo huo Jobi McAnuff.

Reggae Boyz , kwa uwazi, walikuwa tu na furaha kuwa karibu mchezaji huyo wa Barcelona.
Brown, ambaye pia alipata "selfie" na mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, alitupia picha hiyo katika ukurasa wake wa Instagram ikiwa na ujumbe, "Sio matokeo tuliyokuwa tukiyatafuta, lakini nimebahatika kukutana na wachezaji bora duniani na ilikuwa ni hisia kubwa kucheza dhidi yake. Namtakia heri Messi pamoja na Argentina katika sehemu ya mashindano iliyobakia."




Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
WACHEZAJI WA JAMAICA WAFURAHIA KIPIGO, WAOMBA KUPIGA PICHA "SELFIE" NA MESSI...
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment