
Klabu ya Bologna ya nchini Italia ina matumaini ya kumrejesha kwenye ligi ya Sirie A, mshambuliaji Super Mario Balotelli, ambaye ameonyesha kutoyafurahia maisha ya nchini England tangu aliposajiliwa msimu uliopita na klabu ya Liverpool.
Bologna imedhamiria kumsajili Balotelli, huku ikitambua fika klabu ya Sampdoria ipo katika mchakato wa kimazungumzo na viongozi wa Liverpool ili kufanikisha mipango ya usajili wa mshambuliaji huyo.
Uwepo wa klabu hizo mbili za nchini Italia, unaongeza ushawishi kwa mashabiki wa Balotelli kuamini kutakua na uwezekano kwa mchezaji wao kurejea nyumbani na kucheza soka lake kama ilivyo kawaida.

Hata hivyo msukumo wa kuuzwa kwa mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 24, umeendelea kupata kasi baada ya kusajiliwa kwa Christian Benteke Liolo akitokea Aston Villa juma lililopita.
Washambuliaji wengine waliosajiliwa huko Anfield ni, Roberto Firmino pamoja na Danny Ings.
Tayari meneja wa Liverpool Brendan Rodgers alishaeleza hatma ya Balotelli mbele ya waandishi wa habari kwa kusisitiza kwamba mshambuliaji huyo kutoka nchini Italia ana maamuzi ya mwisho wa kubaki ama kuondoka klabuni hapo kwa kutumia uwezo wake binafsi.
Balotelli alisajiliwa na Liverpool akitokea AC Milan kwa ada ya usajili wa pauni milioni 16, na alitarajiwa kufanya mambo makubwa kufuatia kuondoka kwa Luis Suarez, lakini mambo yalikwenda tofauti na kujikuta akifunga mabao machache katika michezo 16 aliyocheza.
Ada ya usajili wa Balotelli kutoka Liverpool tayari imeshatajwa kuwa ni pauni milioni 7.
Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
BALOTELLI MBIONI KUTIMKA ANFIELD
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment