
Meneja wa klabu ya Real Madrid, Rafael Benitez amekataa kumjibu Jose Mourinho baada ya kurushiwa vijembe vilivyogusa maisha yake kisoka pamoja na familia.
Benitez, ambaye kwa sasa yupo mashariki ya mbali (China) sambamba na kikosi chake ambacho kinajiandaa na msimu mpya wa ligi, hakujibu jambo lolote pale alipoulizwa na waandishi wa habari juu ya vijembe alivyorushiwa na Mourinho.
Meneja huyo kutoka nchini Hispania, amesema yeye ni mwanasoka na katu hawezi kuyapa nafasi mazingira ya kipuuzi ambayo yamekua yakitengenezwa na watu wachache, kwa kujitafutia umaarufu duniani.
Amesema kwa sasa ni wakati mzuri kwake kuendelea na harakati za kukiandaa kikosi cha Real Madrid kwa ajili ya mchezo wa kirafiki dhidi ya AC Milan ambao utamsaidia kwenye mipango yake ya kufikia lengo la kufanya vyema msimu ujao wa ligi.

Chokochoko dhidi ya Benitez, zimechagizwa na kauli ya mke wa meneja huyo wa Real Madrid, Montserrat Seara, baada ya kusisitiza mara zote mume wake amekuwa akifanya vyema pale Mourinho alipopita huku akitolea mifano ya timu za Inter, Chelsea na sasa The Galacticos.
Kufuatia msisitizo huo Jose Mourinho hakuwa nyuma badala yake aliamua kurudisha mashambulizi kwa kusema maneno ya kashfa.
Mourinho aliwambia waandishi wa habari akiwa nchini Marekani kwamba, anahisi mke wa Benitez atakuwa amechanganyikiwa kwa namna fulani, kwa sababu mume wake alienda Chelsea kumrithi, Roberto Di Matteo na pia ameenda Real Madrid kumrithi Carlo Ancelotti.
Alisema kazi ambayo Benitez aliirithi kutoka kwake ni Inter Milan pekee, ambapo kwa takribani muda wa miezi sita tu alikiharibu kikosi ambacho kilikuwa bora barani Ulaya kwa kipindi hicho.
Mourinho aliongeza maneno yake kwa kumshauri mke wa Benitez kwa kumtaka aache kuzungumza kumuhusu yeye, kwani anahitaji kuutumia muda wake vizuri kufikiria diet (Mpangilio wa vyakula) ya mumuwe.
Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
BENITEZ: SINA MUDA WA KUMJIBU MPUUZI MOURINHO
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment