
Aliyekua mgombea nafasi ya urais wa shirikisho la soka duniani FIFA, Ali bin Al Hussein amempinga rais wa shirikisho la soka barani Ulaya UEFA, Michel Platini kwa kusema hafai kusimama katika kinyang’anyiro cha kujaza nafasi ya Sepp Blatter kwenye uchaguzi wa mwezi februari mwakani.
Ali bin Al Hussein ambaye ni mtoto wa mfalme wa Jordan, ametoa angalizo hilo baada ya saa 24 kupita, ambazo zilishuhudia Platini akitangaza nia ya kuwania kiti cha uraisi wa FIFA baada ya kupata Baraka kutoka kwa wajumbe wa kamati ya utendaji ya UEFA mwishoni mwa juma lililopita.
Al Hussein amesema Platini hana sifa zilizo thabiti za kuiongoza FIFA ambayo kwa sasa imetapakaa uchafu wa rushwa, hivyo amewataka wadau wa soka duniani kutambua kwamba kuna ulazima kwa baadhi ya viongozi kujipima kabla ya kutangaza nia ya kuwania nafasi kubwa katika taasisi za kidunia.
Hata hivyo Al Hussein hakuweka wazi ni vipi Platini hatoshi katika nafasi hiyo kwa vigezo vya kuzuia rushwa, zaidi ya kusisitiza kuna ulazima kwa baadhi ya watu kujichunguza kwanza kutokana na vitendo vinavyoendelea miongoni mwa watu wanaowazunguuka.
Katika hatua nyingine Al Hussein, bado hajatangaza kama atawania nafasi ya urais kwa mara nyingine tena ama la, hali ambayo inahisiwa huenda ikawa ni hofu kwake baada ya kuona Platini ametangaza nia ya kukitaka kiti cha urais wa FIFA.
Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
MWANA WA MFALME ALI BIN AL HUSSEIN AMPINGA PLATINI
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment