
Kocha wa Torino Giampiero Ventura amethibitisha kwamba dili la kumuuza mlinzi wao Matteo Damian kwa klabu ya Manchester United imekamilika.
Mtandao wa Goal unafahamu kuwa Manchester United imekubali kulipa dau la euro milioni 20 ili kumnasa beki wa kulia mwenye umri wa miaka 25 na inategemewa kutangazwa hivi karibuni.
"Ni kweli, Damian atacheza katika ligi ya Mabingwa akiwa na Manchester United," kocha huyo aliliambia jarida la Sky Sport la Italia.
"Matteo anastahili timu bora na siku zote amekuwa na ndoto ya kuchezea Ligi ya Mabingwa, sasa ni wakati wake.
"Ndani ya kipindi cha miaka minne tangu Damian amejiunga na Torino akitokea AC Milan, tumetoka Serie B na kuweka changamoto kubwa kwa timu zenye ubora wa juu na pia kuwa na muamko wakutaka kushiriki Ligi ya Europa.
"Tumefanya kazi na Damian kwa miaka mingi, nadhani ni wakati muafaka wakumpatia muda wa yeye kufanikisha ndoto zake za kushiriki Ligi ya Mabingwa."
Manchester United pia inamuwania mlinzi wa Argentina Nicolas Otamendi na bado wana matumaini ya kumnasa beki wa kati Sergio Ramos.
Chanzo: Goal.com
July 9,2015
Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
"MANCHESTER UNITED ITAMPATA DAMIAN," KOCHA WA TORINO ATHIBITISHA...
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment