
Baada ya kuwepo na taarifa kwamba, kiungo hodari wa Yanga na nahodha wa timu ya taifa ya Ruanda Haruna Niyonzima kwamba ameitoroka klabu hiyo kufuatia kutoonekana kwa muda mrefu kwenye mazoezi ya mabingwa hao wa ligi kuu Tanzania bara japokuwa likizo kwa wachezaji imekwisha na wachezaji wote wameshariboti na kujiunga na timu. Yanga imelitolea ufafanuzi jambo hilo.
Yanga kupitia kwa katibu wake mkuu Dkt. Jonas Tiboroha imekanusha uvumi huo na kusema kuwa, mchezaji huyo hajaitoroka klabu yao na wanataarifa za kuchelewa kwake kuijunga na kikosi chao ambacho tayari kimeanza mazoezi kwa ajili ya kujiandaa na michuano ya Kagame pamoja ligi kuu msimu ujao.
“Wiki iliyopita Niyonzima alifiwa na mdogoake, mdogoake alikua amekwenda kuogelea ‘somewhere’ bahati mbaya akafariki kwahiyo taarifa tulikuwa tunazo kwamba amefiwa na alikuwa na msib”, amesema Tiboroha.
“Sasa kwa bahati mbaya sana juzi pia wakati yupo kwenye mipango ya kurudi huku, watotowake mapacha ambao wamezaliwa miezi michache iliyopita wakashindwa kutoka ndani ya Ruanda kuja huku (Tanzania) kwasababu walikosa visa na walikuwa hawajapata ‘passport’”, Tiboroha amefafanua.
“Lakini anamaliza kufanya ‘process’ za passport na nafikiri kesho Niyonzima atafika, hakuna ukweli wa maneno kwamba Niyonzima ameitoroka Yanga”, amesisitiza.
Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
YANGA YATOLEA UFAFANUZI SUALA NIYONZIMA KUIKACHA...
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment