
Mshambulizi wa Liverpool na Italia , Mario Balotelli hajarejea kambini Anfield kwa mazoezi ya kabla ya kuanza kwa msimu mpya.
Muitaliano huyo ambaye hakuwa na msimu wa kufana alipojiunga na the Reds anasemekana kuwa alifiwa.
The Reds' walirejea katika kambi ya mazoezi siku ya jumatatu baada ya likizo ndefu ya msimu wa jua.
"ningependa kuwashukuru mashabiki wangu wote''
''Familia yangu inawashukuru pia''alisema mshambulizi huyo machachari.
Balotelli alifunga bao moja pekee katika ligi ya premia

Balotelli mwenye umri wa miaka 24 anatarajiwa kujiunga na kikosi hicho cha Liverpool kabla ya ziara ya kujipima nguvu mashariki ya mbali na Australia.
Tangu ajiunge na the Reds mshambulizi huyo wa zamani wa Manchester City hakunga'ara kama ilivyotarajiwa baada ya kununuliwa kwa kima cha pauni milioni £16m mwezi Agosti.
Alifunga mabao 4 ikiwemo moja pekee katika ligi ya premia na hakuweza kuhakikishiwa nafasi ya timu ya kwanza licha ya kutokuwepo kwa nyota kutoka Uruguay Luis Suarez.
Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
MCHEZAJI WA LIVERPOOL MARIO BALOTELLI HAJAREJEA KAMBINI LIVERPOOL...
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment