Nyota wa Liverpool Raheem Sterling ndiye mchezaji chipukizi anayethaminiwa zaidi barani Ulaya kwa mujibu wa utafiti.
Kandanda
1. Raheem Sterling (Liverpool) £35m 7. Mateo Kovacic (Inter Milan) £18.5m
2. Marquinhos (Paris St-Germain) £27.8m 8. Jose Gaya (Valencia) £18.3m
3. Memphis Depay (Manchester United) £23.8m 9. Luke Shaw (Manchester United) £18m
4. Domenico Berardi (Sassuolo) £21.6m 10. Aymeric Laporte (Athletic Bilbao) £17m
5. Jose Gimenez (Atletico Madrid) £21.4m 16. John Stones (Everton) £12m
6. Hakan Calhanoglu (Bayer Leverkusen) £19.4m 19. Calum Chambers (Arsenal) £10.6m
Raia huyo wa Uingereza ambaye harakati za kuhamia Manchester City, zilitumbukia nyong'o amekadiriwa kuwa mwenye thamani ya pauni milioni 35 na kampuni ya utafiti ya Soccerex inayochapisha Orodha
ya wachezaji wenye thamani ya juu ama 20 Football Value Index.
Manchester City ilikuwa imeweka dau la pauni milioni £40 lakini ombi lao likakataliwa na Liverpool.
Mlinzi wa Manchester United, Luke Shaw ameorodheshwa katika nafasi ya 9, John Stones wa Everton ameorodheshwa wa 16 huku kiungo wa Arsenal Calum Chambers akiorodheshwa katika nafasi ya 19.
Kampuni hiyo ya Soccerex imefanya utafiti huo miongoni mwa wachezaji wasiozidi umri wa miaka 21 wanaocheza katika ligi za bara ulaya.
Inatumia vipengee kama umri,nafasi wanayocheza uwanjani,Klabu,urefu wa Kandarasi,mechi walizochezea timu zao za taifa,mechi walizocheza,mabao waliofunga,majeraha na ubora wao kitalanta.
''tukiangalia kwa kina vipengee hivi vyote tunaweza kutathmini uwezo na thamani ya mchezaji.''
''Hivyo vyote ndivyo vilitusaidia kubaini kuwa Sterling ndiye mchezaji bora na mwenye thamani ya juu zaidi barani ulaya kwa sasa.'' alisema bwana Esteve Calzada

Mlinzi wa Paris St-Germain ya Ufaransa ambaye ni raia wa Brazil Marquinhos ameorodheshwa katika nafasi ya pili na thamani ya pauni milioni £27.8.
Mchezaji mpya wa Manchester United vilevile ye Uingereza Memphis Depay aliyegharimu kitita cha pauni milioni £31 ameorodheshwa katika nafasi ya tatu akiwa na thamani ya pauni milioni £23.8.
Calzada anasema kuwa sheria iliyowekwa na shirikisho la soka la Uingereza ambayo inazilazimisha vilabu vya Uingereza kuwa na takriban wachezaji 8 raia wa Uingereza imeongeza maradufu thamani ya wachezaji waingereza.
Wachezaji 4 katika orodha hiyo ni raia wa Uingereza huku9 kati ya 20 bora wakitarajiwa kucheza katika ligi kuu ya Uingereza msimu ujao.
Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
STERLING: MCHEZAJI ANAYETHAMINIWA ZAIDI ULAYA...
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment