
Liverpool walikamilisha usajili wenye gharama ya pauni milioni 16 kumnyaka nyota wa Italia kutoka katika kilabu cha AC Milan Mario Balotelli ambaye ameshindwa kuwika katika klabu ya Liverpool na kwa sasa hali imekuwa mbaya kwa mchezaji huyo aliyeambiwa abaki akifanya mazoezi peke yake baada ya kilabu hicho kuelekea Finland kwa ajili ya mchezo wa kirafiki dhidi ya HJK.
Haya yote yamezidi kumkumba mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24 baada ya kutuma ujumbe kumsifia mchezaji Raheem Sterling aliyetimka kilabuni hapo kuelekea Manchester City na kufanikiwa kutupia katika mchezo wake wa kwanza katika klabu yake hiyo mpya.
Lakini muonekano huu unadhihirisha kuwa maisha ya Mario katika kilabu hicho yamefikia ukingoni baada tu ya msimu mmoja tangu ajiunge kutokea AC Milan ambapo amefanikiwa kutupia magoli 4 tu katika michezo 28 aliyotokea, huku goli moja kati ya magoli hayo likiwa ni la Ligi Kuu.

Bosi wa Liverpool Brendan Rodgers alisema wiki iliyopita huko Kuala Lampur ambapo walishiriki ziara yao ya maandalizi ya msimu kuwa amemuachia Mario mwenyewe kuamua maisha yake ya baadae.
Bologna ni klabu ya Serie A inayomuwania Balotelli, ambaye ana miaka miwili iliyosalia katika mkataba wake ambao analipwa pauni 90,000 kwa wiki, lakini Liverpool hawajapokea ofa rasmi yoyote kwa ajili ya mshambuliaji huyo mtukutu.
Imeripotiwa kuwa Balotelli amekuwa akifanya mazoezi kila siku, pamoja na beki wa kushoto wa Hispania Jose Enrique na Fabio Borini ambao wanaonekana kutokuwa na nafasi katika kikosi cha Brendan.
Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
HALI IMEZIDI KUWA MBAYA KWA MARIO BALOTELLI
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment