
Je, Sunday Oliseh ndiye atakaye kuwa kocha mpya wa Nigeria ?
BBC imebaini kuwa kiungo huyo wa kati wa zamani wa Super Eagles ya Nigeria, Sunday Oliseh anafanya mazungumzo na shirikisho la soka la Nigeria NFF kwa nia ya kutangazwa kuwa kocha wa timu ya taifa ya Nigeria.
Nahodha huyo wa zamani wa Super Eagles mwenye umri wa miaka 40 aliingoza timu hiyo katika mechi 63 za kimataifa.
Kwa mujibu wa mwandani wetu anatarajiwa kutangazwa karibuni kuwa kocha mpya.
NFF ililazimika kufanya bidii ilikuziba pengo lililoachwa wazi na Stephen Keshialiyefutwa kazi mwishoni mwa juma.
Oliseh alikuwa miongoni mwa kikosi cha taifa kilichotwaa kombe la mataifa ya Afrika mwaka wa 1994 na kisha nishani ya dhahabu ya olimpiki mwaka wa 1996 .
Oliseh vilevile alikuwa katika kikosi kilichoiwakilisha Nigeria katika kombe la dunia la mwaka wa 1994 na 1998.

Super eagles ilifuzu katika mkumbo wa 16 bora katika mashindano hayo mawili.
Oliseh anakumbukwa kwa bao lililoisaidia Nigeria kuibana Uhispania katika mechi za makundi.
Kizazi chake kinatajwa na wengi kuwa maarufu zaidi katika historia ya soka ya nchi hiyo kwa pamoja na Jay-Jay Okocha, Nwankwo Kanu na Finidi George.
Oliseh amekuwa akihudumu kama mtangazaji wa kandanda mbali na kuwa mshauri wa FIFA wa maswala ya kiufundi.

Japokuwa Oliseh hana tajriba ya kufunza timu ya taifa aliwahi kuifunza timu ya daraja la pili la Ubeljiji Vervietois kati ya mwaka wa 2008 na 2009.
Iwapo atatangazwa kuwa kocha wa Nigeria Oliseh atachukua hatamu kutoka kwa mkurugenzi wa kiufundi wa NFF Shaibu Amodu na kocha msaidizi Salisu Yusuf.
Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
SUNDAY OLISEH KUWA KOCHA WA NIGERIA...
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment