MANCHESTER UTD WANAJARIBU KUMSAJILI RONALDO:
Klabu ya Manchester United wanajaribu kumrejesha Old Trafford mchezaji wa Real Madrid Cristiano Ronaldo. Mashetani hao wekundu wana kazi ya kufanya dili ambalo litakuwa rekodi mpya klabuni hapo huku wakiwa na nia ya kusajili wachezaji wenye viwango vya juu majira haya.
Chanzo: Manchester Evening News
Alhamisi, 7/23/2015 20:05
PSG WAMEKUBALI ADA YA DI MARIA YENYE THAMANI YA EURO 65 MILIONI:
PSG wamekubaliana na Manchester United ada ya euro milioni 65 sawa na pauni milioni 45.5 kwa ajili ya kumsajili Angel Di Maria. Mchezaji huyo wa Kiargentina ataungana na wachezaji wenzake wa timu yake mpya huko USA wikiendi hii.
Chanzo: France Football
Alhamisi, 7/23/2015 20:37
SAMPER AMEPANGA KUZUNGUMZA NA BARCA HUKU KUKIWA NA UVUMI TOKA KWA ARSENAL:
Sergi Samper anajipanga kuzungumza na klabu yake ya Barcelona kuhusiana na mustakabali wake huku kukiwa na uvumi kutoka katika kilabu cha Arsenal ambao wanamtazama mchezaji huyo kijana kama mbadala wa Mikel Arteta kilabuni hapo.
Chanzo: Daily Express
Alhamisi, 7/23/2015 19:37
WEST HAM NA EVERTON VINAMUWANIA HALILOVIC KWA MKOPO:
Barcelona wanatazamia kumruhusu Alen Halilovic kujiunga kwa mkopo huku wote Everton na West Ham wakimuwania mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 19.
Chanzo: Daily Mail
Alhamisi, 7/23/2015 19:00
MADRID HAITOMUUZA RAMOS:
Raisi wa kilabu cha Real Madrid Florentino Perez atafanya mazungumzo na Sergio Ramos wikiendi hii na atamwambia beki huyo kuwa kilabu hicho hakitamuuza majira haya.
Chanzo: The Gurdian
Alhamisi, 7/23/2015 17:18
WELBECK KWENYE RADA YA BESIKTAS:
Besiktas wanatazamia kumnyatia mshambuliaji wa kilabu cha Arsenal Danny Welbeck.
Chanzo: Fanatik
Alhamisi, 7/23/2015 16:32
MADRID WATAMJUMUISHA NAVAS TU KWENYE DILI LA DE GEA:
Real Madrid wameimbia klabu ya Manchester United kuwa hawatolipa zaidi ya euro milioni 25 sawa na pauni milioni 17.6 kwa ajili ya kuipata saini ya David De Gea na watamjumuisha Keylor Navas tu kwenye dili hilo.
Chanzo: ABC
Alhamisi, 7/23/2015 15:45
NORWICH INAMUWANIA ALONSO:
Norwich City wanajiandaa kutoa kitita cha euro milioni 3 sawa na pauni milioni 2.1 kumnyakuwa mlinzi wa klabu ya Fiorentina Marcos Alonso.
Chanzo: Mediaset
Alhamisi, 7/23/2015 15:00
PSG WAMETOA DAU KWA AJILI YA LACAZETTE:
Paris Saint-Germain wamewasilisha euro milioni 38 (pauni milioni 26.8) kwa ajili ya kumnyakuwa mshambuliaji wa Lyon Alexandre Lacazette.
Chanzo: Gazzetta dello Sport
Alhamisi, 7/23/2015 14:57
WEST BROM KWENYE MAZUNGUMZO NA DIABY:
West Brom wapo kwenye mazungumzo na kiungo wa zamani wa Arsenal Abou Diaby.
Chanzo: Birmingham Mail
Alhamisi, 7/23/2015 13:44
TOTTENHAM, WEST HAM NA ASTON VILLA KWENYE VITA YA BOLASIE:
Tottenham, West Ham na Aston Villa wote wameulizia upatikanaji wa nyota wa Crystal Palace Yannick Bolasie na The Eagles hao wanatarajia kupokea dau angalau kutoka katika vilabu viwili kwa ajili ya winga huyo.
Chanzo: Sky Sports
Alhamisi, 7/23/2015 12:25
LIVERPOOL WAMRUDIA PEDRO:
Huku Manchester United wakiwa katika mbio za kumnyakuwa Pedro, Liverpool wameingia tena kwenye mbio hizo za kumsajili mchezaji huyo kutoka Barcelona.
Chanzo: Mundo Deportivo
Alhamisi, 7/23/2015 11:13
LAZIO WAMEKATAA DAU LA MAN UTD KWA BIGLIA:
Lazio wamekataa dau la euro milioni 25 (pauni milioni 17.5) lililotolewa na kilabu cha Manchester United kwa ajili ya kumpata Lucas Biglia.
Chanzo: Corriere dello Sport
Alhamisi, 7/23/2015 10:24
ARSENAL WANAANDAA DAU LA ISCO:
Arsenal wapo tayari kutoa ofa kwa nyota wa Real Madrid Isco. Mchezaji huyo wa Kihispania amepambana kujipatia namba Bernabeu na inaweza kumfanya atimke klabuni hapo, huku Arsene Wenger akitazamia kuiba kile Chelsea na Man City wakitazamia.
Chanzo: Daily Star
Alhamisi, 7/23/2015 09:48
CHELSEA WANAFANYA MAZUNGUMZO NA CALLEJON:
Chelsea wanatarajia kumnyatia mchezaji wa Napoli Jose Callejon na wamefungua mazungumzo na timu hiyo ya Italia. Maurizio Sarri yupo tayari kumuondoa mchezaji huyo wa Hispania, amabaye atagharimu pauni milioni 10.4, na wanatumaini kumleta Mohamed Salah kama sehemu ya dili hilo.
Chanzo: Metro
Alhamisi, 7/23/2015 09:44
VARANE KUMFANYA RAMOS KUBAKI MADRID:
Real Madrid wameamua kumbakiza klabuni hapo beki wao wa kati Sergio Ramos kutokana na hali ya Raphael Varane kutokuwa fiti. Mchezaji huyo wa kimataifa wa Ufaransa ana matatizo ya goti ya muda mrefu, yaliyomfanya akose mazoezi msimu uliopita, kwa hiyo Ramos hatoruhusiwa kutimka klabuni hapo.
Chanzo: El Confidencial
Alhamisi, 7/23/2015 09:27
ARSENAL INAMNYEMELEA LEWANDOWSKI:
Arsenal wapo tayari kudondosha sarafu yao kwa mshambuliaji wa Bayern Munich Robert Lewandowski kama dili la kumnyakuwa Karim Benzema litashindikana. Arsene Wenger anajaribu kumleta nyota huyo wa Real Madrid, lakini anatazamia kuwa raia huyo wa Poland kuwa mbadala wa dili hilo.
Chanzo: Metro
Alhamisi, 7/23/2015 09:26
INTER WANATARAJIA KUMSAJILI JOVETIC:
Inter wamefikia makubaliano na klabu ya Manchester City juu ya uhamisho wa Stevan Jovetic kwa dili la miaka miwili ya mwanzo ya mkopo, pamoja na kuwa na wajibu wa kumnyakuwa moja kwa moja kwa ada ya euro milioni 20.
Chanzo: Corriere dello Sport
Alhamisi, 7/23/2015 07:29